Tuesday, June 12, 2012

TUNABADILI JINA

Nawashukuru wadau wote wa NGARALIVE kwa kuendelea kuwa karibu na BLOG yenu ili kupata taarifa mbali mbali zinazojili wilayani kwetu.Hata hivyo nasikitika kuwataarifu kuwa kwa sasa nabadili jina na maudhui ya BLOG hii.Nimelazimika kufanya hivyo kutokana na kuhamisha makazi yangu.Awali nilikuwa wilayani Ngara lakini kwa sasa nahamia Mkoani MWANZA kikazi,hivyo haitakuwa rahisi mimi kupatra kile kinachojiri NGARA kwa wakati husika.
Kwa hali hiyo nitakuwa naweka taarifa za kitaifa,japo na zile za NGARA zitakuwa zinapewa kipaumbele,kwa hiyo tegemeeni kuona mabadiliko ya taarifa kutoka NGARALIVE inayobadilika kuwa DOXLIN JASSON.BLOGSPOT.COM
ASANTENI...........

Wednesday, May 16, 2012

CAPTAIN BRIAN BGOYA AFARIKI DUNIA

Captain Brian Niyimpa Bgoya(pichani) amefariki dunia katika hospitali ya HINDU MANDAL jijini Dar es Salaam tarehe 13 MAY mwaka huu.

Mazishi yatafanyika siku ya Jumamosi MAY 15 nyumbani kwao Mubinyange Ngara ambapo mwili wa marehemu unatarajiwa kufikishwa Ngara siku ya Ijumaa.

NGARA LIVE INATOE POLE KWA WOTE WALIOFIKWA NA MSIBA HUO

Wednesday, May 9, 2012

WILAYA YA NGARA YAPATA MKUU WA WILAYA MPYA

Wilaya ya Ngara imepangiwa Mkuu wa Wilaya mpya,atakayechukua nafasi ya Kanali Mstaafu Salum Nyakonji.
Kwa mujibu wa uteuzi mpya wa Wakuu wa Wilaya,nafasi hiyo hapa wilayani Ngara itachukuliwa na COSTANTINE J.KANYASU.
Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Ngara Kanali Mstaafu Salum Nyakonji,kushoto kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kanali Mstaafu Fabian Massawe
Hata hivyo taarifa hiyo ya awali haikueleza kama kuna kituo kingine alichopangiwa KANALI NYAKONJI.

Wafuatao ndio Wakuu wapya wa wilaya na vituo vyao vya kazi
1. Novatus Makunga Hai
2. Mboni M. Mgaza Mkinga
3. Hanifa M. Selungu Sikonge
4. Christine S. Mndeme Hanang
5. Shaibu I. Ndemanga Mwanga
6. Chrispin T. Meela Rungwe
7. Dr. Nasoro Ali Hamidi Lindi
8. Farida S. Mgomi Masasi
9. Jeremba D. Munasa Arumeru
10. Majid Hemed Mwanga Lushoto
11 Mrisho Gambo Korogwe
12. Elias C. J. Tarimo Kilosa
13. Alfred E. Msovella Kiteto
14. Dkt. Leticia M. Warioba Iringa
15. Dkt. Michael Yunia Kadeghe Mbozi
16. Mrs. Karen Yunus Sengerema
17. Hassan E. Masala Kilombero
18. Bituni A. Msangi Nzega
19. Ephraem Mfingi Mmbaga Liwale
20. Antony J. Mtaka Mvomero
21. Herman Clement Kapufi Same
22. Magareth Esther Malenga Kyela
23. Chande Bakari Nalicho Tunduru
24. Fatuma H. Toufiq Manyoni
25. Seleman Liwowa Kilindi
26. Josephine R. Matiro Makete
27. Gerald J. Guninita Kilolo
28. Senyi S. Ngaga Mbinga
29. Mary Tesha Ukerewe
30. Rodrick Mpogolo Chato
31. Christopher Magala Newala
32. Paza T. Mwamlima Mpanda
33. Richard Mbeho Biharamulo
34. Jacqueline Liana Magu
35. Joshua Mirumbe Bunda
36. Constantine J. Kanyasu Ngara
37. Yahya E. Nawanda Iramba
38. Ulega H. Abadallah Kilwa
39. Paul Mzindakaya Busega (mpya)
40. Festo Kiswaga Nanyumbu
41. Wilman Kapenjama Ndile Mtwara
42. Joseph Joseph Mkirikiti Songea
43. Ponsiano Nyami Tandahimba
44. Elibariki Immanuel Kingu Kisarawe
45. Suleiman O. Kumchaya Tabora
46. Dkt. Charles O. F. Mlingwa Siha
47. Manju Msambya Ikungi (mpya)
48. Omar S. Kwaangw’ Kondoa
49. Venance M. Mwamoto Kibondo
50. Benson Mpesya Kahama
51. Daudi Felix Ntibenda Karatu
52. Ramadhani A. Maneno Kigoma
53. Sauda S. Mtondoo Rufiji
54. Gulamhusein Kifu Mbarali
55. Esterina Kilasi Wanging’ombe (mpya)
56. Subira Mgalu Muheza
57. Martha Umbula Kongwa
58. Rosemary Kirigini Meatu
59. Agness Hokororo Ruangwa
60. Regina Chonjo Nachingwea
61. Ahmed R. Kipozi Bagamoyo
62. Wilson Elisha Nkhambaku Kishapu
63. Amani K. Mwenegoha Bukombe
64. Hafsa M. Mtasiwa Pangani
65. Rosemary Staki Senyamule Ileje
66. Selemani Mzee Selemani Kwimba
67. Lt. Col. Ngemela E. Lubinga Mlele (mpya)
68. Iddi Kimanta Nkasi
69. Muhingo Rweyemamu Handeni
70. Lucy Mayenga Uyui

Tuesday, May 8, 2012

AJALI YAUA WAWILI K 9


Mteremko wa K 9 umezidi kuwa tishio hasa kwa madereva wa maroli baada ya hivi karibuni lori moja kufail break kisha kuacha njia na kuua watu wawili papo hapo.

Dereva wa Lori hilo lililokuwa likitokea Dar es Salaam kuelekea Burundi,ni mmoja kati ya waliopoteza maisha.
Mwingine ni mwendesha piki piki ambaye ni mkazi wa kijiji cha Kasharazi,yeye alikuwa barabarani ambapo gari hilo lilimpitia katika harakati za kuacha njia.

hiyo ni sehemu ya CABIN ya lori hilo
kwa mbali hiyo inayoonekana ndiyo piki piki iliyogongwa ikiwa chini ya gari hilo
hivyo ndivy lilivyokuwa
hilo ndilo container la gari hilo,lenyewe lilichomoka na kuporomoka zaidi ya mita mia moja hamsini,na ndani ya container hilo kulikuwa na gari jipya aina ya FUSO
Utingo wa Lori hilo alishuka kuweka kigingi baada ya kuona kuwa limefail break,hivyo yeye hakuweza kupata jeraha lolote.

Tuesday, May 1, 2012

HIKI NDICHO SHULE ZETU ZA NGARA ZILICHOKIVUNA KATIKA MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2012


S0611 KABANGA SECONDARY SCHOOL

DIV-I = 1 DIV-II = 9 DIV-III = 36 DIV-IV = 10 FLD = 1 

+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++

S0397 RULENGE SECONDARY SCHOOL

DIV-I = 1 DIV-II = 4 DIV-III = 19 DIV-IV = 10 FLD = 1 

 ++++++++++++++++++++++++++++++++++++++

S4419 LUKOLE SECONDARY SCHOOL

DIV-I = 1 DIV-II = 25 DIV-III = 59 DIV-IV = 4 FLD = 0 

+++++++++++++++++++++++++++++++++

 

Friday, April 20, 2012

HUU NDIO USAFIRI WETU NGARA

Kwa wale waliozoea usafiri wa mijini,hali inakuwa tofauti wanapokuja Ngara kqwani hali ya usafiri iko tofauti kabisa.

Gari ambayo kwa sehemu nyingine hupakia watu wasiozidi wanne,hapa kwetu inaweza kupakia watu zaidi ya 12,huku wengine wakikaa kwenye buti(sehemu ya kuwekea mizigo).

Nauli kutoka Ngara mpaka Kabanga ni shilingi elfu mbili kwa mtu mmoja,na kuna wakati wanapanda watu 15 kwenye hicho hicho kigari kidogo chenye uwezo wa kubeba abiria wanne.

Seat au kiti anachokalia dereva,hulazimika kukaa watu wawili kitu ambacho ni hatari sana kwani kinaweza kusababisha ajali.
hii ndiyo hali halisi

Kuna watu wamekuwa wakileta HIACE lakini muda c mrefu hukata tamaa kutokana na abiria kutaka kupanda gari ambalo halikai muda mrefu stand likisubiri abiria

BIASHARA YA MATUNDA ITAWANUFAISHA WENGI SANA NGARA

Kwa sasa wananchi wengi wa wilaya ya Ngara wamesitisha shughuli zao za kawaida na kuhamia katika biashara ya kusafirisha matunda kama vile maparachichi na ndizi za kisasa au ndizi kubwa.

Matunda hayo husafirishwa kwenda mikoa ya kanda ya kati (Dodoma na Singida)ambapo mfanyabiashara anaweza kupata faida ya zaidi ya shilingi elfu arobaini kwa gunia moja.

Gunia moja la maparachichi linaweza kupatikana katika vijiji vya wilayani Ngara kwa gharama isiyozidi  elfu kumi,ambapo bei ya kusafirisha gunia moaj kufika Dodoma ni shilingi elfu tano,na mzigo ukishafika Dodoma unauzwa kwa bei isiyopungua elfu hamsini kwa gunia moja,na mzigo ukifika Dodoma hauzungushwi,ndani ya masaa 12 mzigo unakuwa umekwisha tena kwa kugombaniwa.

je,ukipakia gunia ishirini unapata faida ya bei gan?

mzigo ukipakiwa kwenye lori kwa ajili ya kusafirishwa kuelekea Dodoma
Hali ya usafiri ndiyo rahisi sana kwani kuna maroli mengi yanatoka Burundi kwenda DAR,so hii ni biashara ambayo watu wengi wanaidharau lakini inalipa saaana.

Wednesday, April 18, 2012

JAMBAZI AUWAWA NA POLISI


Diwani wa kata ya Kabanga MH SAID SOUD
Jeshi la polisi wilayani Ngara limemuua mtu anayedhaniwa kuwa jambazi aliyekuwa na bomu la kutupwa kwa mkono

Diwani wa kata ya Kabanga Bw. Said Ramadhani Soud amesema tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo katika kijiji cha Nzaza baada ya kundi la majambazi  kutoka Burundi kuvamia katika kijiji cha Murukukumbo

Amesema jeshi la polisi kituo cha kabanga lilipata taarifa hizo ambapo waliwafuatilia na kumuua jambazi huyo baada ya tukio la kurushiana risasi na majambazi hao.

Amesema jambazi aliyeuwawa amefahamika kwa jina la Erick Ndabiholele mwenyeji wa wilaya ya Murama nchini Burundi

Amesema Polisi wamepata vitu vyenye thamani ya shilingi laki mbili ikiwa ni pamoja na simu tatu za mkononi zilizokuwa zimeibwa na watu hao

Kata ya Kabanga imekuwa ikikumbwa sana na vitendo vya ujambazi wa kutumia silaha siku za hivi karibuni,ambapo zaidi ya watu wawili wameuwawa na majambazi hao tangu mwanzoni mwa mwaka huu,na inasemekana majambazi hao wanatoka nchi jirani ya Burundi

Tuesday, April 17, 2012

AMBULANCE NGARA

Halmashauri ya wilaya ya Ngara imenunua piki piki za magurudumu matatu zitakazokuwa zikifanya huduma ya kuwasafirisha wanawake wajawazito kutoka vijijini kuwapeleka sehemu za barabarani ambapo watakuwa wakichukuliwa na magari kuelekea katika hospitali kubwa za wilaya kwa ajili ya kupatiwa huduma za kiafya.

Akiongea na NGARALIVE Kaimu Mganga Mkuu wa wilaya ya Ngara Dk.David Mapunda,amesema piki piki hizo tatu zitapangiwa vituo ambavyo zitakuwa zikikaa,japo kwa sasa vityuo hivyo bado havijabainishwa.

mojawapo ya piki piki hizo ikiwa imeegeshwa katika hospitali ya Nyamiaga ikisubiri kupangiwa kituo.Hii itafika kweli Ntobeye kupitia njia ya Murgwanza?
Dk.Mapunda ameongeza kuwa piki piki hizo ni kwa ajili ya wajawazito pekee tofauti na dharula nyingine zinazoweza kujitokeza

MVUA SIKU TATU MFULULIZO

Eneo kubwa la wilaya ya Ngara kwa siku tatu mfululizo limekuwa likitawaliwa na hali ya hewa ambayo sio nzuri sana.

Asubuhi ukiamka ukungu umetanda sehemu zote na manyunyu yasiyoonyesha dalili ya kukatika.

Hii imepelekea baadhi ya watu kusimamisha shughuli zao sanasana wale wa usafiri wa boda boda na sekido.

Hiyo ndo hali halisi inayoendelea hapa Ngara ambapo kwa muda wa siku tatu jua limekuwa adim sana.

BREAAKING NEEEWWZZZZ

ALEX GASHAZA ATANGAZA KUGOMBEA NAFASI YA MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI WILAYA YA NGARA.

Kada wa Chama cha Mapinduzi CCM wilayani Ngara  Bw Alex Gashaza ametangaza rasmi kugombea uenyekiti wa wilaya wa chama hicho.

Bw.Gashaza ambaye amewahi kushiriki katika chaguzi kadhaa za ubunge wa jimbo la Ngara kupitia tiketi ya CCM mara mbili na mara moja kupitia tiketi ya NCCR Mageuzi,ameweka uamuzi huo hadharani katika kikao cha madiwani wa chama cha Mapinduzi kilichofanyika katika ofisi za CCM mjini Ngara.

Uchaguzi wa nafasi mbali mbali ndani ya CCM unafanyika mwaka huu ambapo kwa hivi sasa nafasi hiyo ya mwenyekiti inashikiliwa na Bi.Helena Adrian ambaye anamiliki shule ya RHEC iliyoko Rulenge

Monday, April 16, 2012

WANAFUNZI SITA TU DARASA ZIMA

jengo la utawala la shule ya sekondari MCHUNGAJI MWEMA
Katika hali isiyokuwa ya kawaida shule ya Sekondari inayomilikiwa na kanisa la Anglikana dayosisi ya Kagera,MCHUNGAJI MWEMA,Imeonekana kupoteza kabisa mvuto kwa jamii baada ya shule hiyo kuwa na wanafunzi sita peke yao walioingia kidato cha kwanza mwaka huu shuleni hapo.

wanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya sekondari MCHUNGAJI MWEMA wakiendelea na mjadala wa kimasomo darasani
Habari zilizoifikia NGARALIVE zinasema kuwa uhaba huo wa wanafunzi wanaojiunga na shule hiyo umepelekewa na matokeo mabovu ya kidato cha nne kwa mwaka jana hali ambayo imewakatisha tamaa wazazi.


Nao wanafunzi wa shule hiyo wamesema kuwa hali hiyo inachangiwa na kutokuwepo na maelewano mazuri kati ya waalimu wa shule hiyo na uongozi wa Dayosisi ya Kagera ambao ndio wamiliki wa shule hiyo.

LORI LAANGUKA,LAFUNGA BARABARA IENDAYO BURUNDI



Zaidi ya Malori 40 yaliyokuwa yakipeleka mizigo katika nchi za Burundi na Jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo,yamejikuta yakikwama kwa muda wa masaa zaidi ya 18 katika kijiji cha Murugarama baada ya Lori moja wapo kuanguka na kufunga barabara.

Lori hilo lenye namba za usajiri T 700 BFS lilianguka majira ya saa nane mchana siku ya jumapili April 15 katika kijiji cha Murugarama eneo la Njiapanda ya Rulenge,ambapo lilikuwa likipeleka mahindi nchini Burundi,na baada ya kuanguka lilifunga barabara hiyo hali iliyopelekea magari mengi hasa malori kukosa njia ya kupita kwa masaa kadhaa.

Watu walioshuhudia ajali hiyo wamesema kuwa chanzo chake ni mwendo wa kasi wa gari hilo,pamoja na mvua iliyokuwa ikinyesha kwa muda mrefu katika eneo hilo na kusababisha utelezi.

Hata hivyo watu waliokuwa katika gari hilo walisalimika ambao ni dereva na utingo.

Gari hilo awali likuwa likimilikiwa na Bw.Tenth Maruhe mkazi wa mjini Ngara kabla ya kuliuza kwa Mbarakk wa Biharamulo.

jitihadazikiendelea za kuliondoa barabarani
Baada ya madereva hao kuona hakuna jitihada zozote zinazofanywa na mamlaka husika kuondoa gari hilo barabarani,walishirikiana wao wenyewe na kulitoa ambapo shughuli za usafirishaji katika barabara hiyo zimelejea katika hali ya kawaida.
hivi ndivyo lilivyokaa baada ya kuanguka

wananchi wakishirikiana kuinua tela la lori hilo
Ajali hiyo ni ya pili kutokea katika eneo hilo kwa kipindi cha miezi miwili,ambapo mwezi wa pili watu wawili walipoteza maisha baada ya kugongwa na roli katika eneo hilo hilo.

Thursday, March 29, 2012

WIKI YA MAJI

Askofu wa kanisa la Anglikana dayosisi ya Kagera Dk.Aron Kijanjali akipanda mti rafiki wa maji katika chanzo kipya cha maji safi cha Mubwilinde,baada ya kuzindua mradi huo.
Katibu wa TUMAINI FUND ambao ndio wamefanikisha ujenzi wa mradi wa maji safi katika kijiji cha Mubwilinde Bw.David Kibenza,akipanda mti rafiki wa maji kando ya chanzo hicho mara baada ya Askofu Kijanjali kuufungua mradi huo.
Wanafunzi wa shule ya msingi Mubwilinde wakitoa burudani kwa watu waliohudhuria uzinduzi wa mradi wa maji safi katika kijiji cha Mubwilinde

WIKI YA MAJI

Askofu wa kanisa la Anglikana dayosisi ya Kagera Dk.Aron Kijanjali akiwaongoza mamia ya wakazi wa kijiji cha Mubwilinde katika sala kabla ya kuzindua mradi wa maji safi kwa wakazi wa kijiji hicho.Mwanzo kushoto ni Mratibu wa mradi huo ambaye ni katibu wa mfuko wa Tumaini Bw.David Kibenza
Askofu wa kanisa la Anglikana dayosisi ya Kagera Dk.Aron Kijanjali akifungua mradi wa maji katika kijiji cha Mubwilinde kata ya Bukiriro wilayani Ngara.Mradi huo umejengwa kwa ufadhili wa kanisa hilo kupitia Mfuko wa Tumaini.
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Mubwilinde ambao pia watanufaika na mradi huo wakifuatilia kwa makini wakati Askofu Kijanjali alipokuwa akifungua mradi huo.
Wananchi wa kijiji cha Mubwilinde wakifurahia kwa ngoma baada ya kujengewa mradi wa maji safi na salama

Monday, March 26, 2012

WIKI YA MAJI EXCLUSIVE

Maadhimisho ya wiki ya maji wilayani Ngara yalimalizika wiki iliyopita kwa Mkuu wa wilaya ya Ngara Kanali msitaafu Salum Nyakonji kuwataka wananchi wote wanaofanya shughuli za kibinadamu kando mwa vyanzo vya maji kusitisha shughuli hizo mara moja vinginevyo nguvu ya sheria itatumika kwa wale watakaokaidi agizo hilo.


Akitoa hotuba kwa niaba ya Mkuu wa wilaya ya Ngara Salum Nyakonji,Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Ngara Bw.John Nshimimana alisema kuwa serikali wilayani Ngara iko na wananchi bega kwa bega ili kuhakikisha wananchi wote wa wilaya hiyo wanapayta maji safi na salama.

mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Ngara Mh.John Nshimimana  akizindua tenki la maji kwa niaba ya mkuu wa wilaya katika kata ya Ntobeye,kulia ni diwani wa kata hiyo Mh.John Ruzige.
wanafunzi wa shule ya msingi Ntobeye wakitumbuiza katika kilele cha wiki ya maji
Hao ni wanasanaa kutoka katika kikundi cha Sanaa Kirushya,akina Baba Mpito na mama Mpito ambao wavuta hisia za umati wa watu waliokusanyika katika viwanja vya shule ya msingi Ntobeye katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya maji.

Maadhimisho hayo yalizinduliwa katika kijiji cha Ntelungwe kata ya Nyamiaga,na baada ya hapo zilifuatia shughuli mbali mbali za kimaendeleo katika sekta ya maji wilayani kote,ikiwa ni pamoja na kukagua miradi ya maji na kuzindua miradi hiyo.

Tuesday, March 20, 2012

   HATA SISI TUMO
Swala la utandawazi limeonekana kuingia sehemu kubwa ya dunia hata vijijini ambako zamani walikuwa wakipata habari baada ya mwezi mmoja.

Kwa sasa hali ni tofauti kwani wananchi wengi wamepata uwezo wa kumiliki vifaa vya habari kama vile Radio hata madish kama Camera yetu ilivyokuta huko katika kijiji cha Chivu.

Hii ni nyumba iliyokutwa tulioiona huko Chivu na wanamiliki satellite dish kwa ajili ya kupata kianchoendelea duniani.


hii ni nyumba iliyoko huko katika kijiji cha chivu
MAADHIMISHO YA WIKI YA MAJI WILAYANI NGARA.

Wananchi wilayani hapa,wametakiwa kutumia maji safi katika shughuki mbali mbali na sio kupikia tu.
Kauli hiyo imetolewa na Katibu tawala wa wilaya ya Ngara Bw.Erasmus Rugarabamu,alipokuwa akikabidhi mradi wa maji safi katika kijiji cha Mukalinzi kata ya Muganza wilayani Ngara.

Ikiwa ni katika maadhimisho ya wiki ya maji,Bw.Rugarabamu amesema kuwa wananchi wengi wa wilaya hiyo,wamekuwa wakitumia maji safi kwenye kupikia tu,wakati wao na watoto wao wamekuwa hawajali suala la usafi kwa kufulia nguo maji mengi yanayopatikana wilayani humo.

katibu tawala wa wilaya ya Ngara Bw.Erasmus Rugarabamu,akizindua rasmi
mradi wa maji safi katika kijiji cha mukalinzi kata ya Muganza.
Kwa upande wao wananchi wa kijiji hicho wameishukuru serikali kuweza kuwafikishia mradi wa maji safi,kwani awali walikuwa wakittumia kisima ambacho kilikuwa katika hali mabaya sana kiafya.Mradi huo umejengwa na shirika la TWESA kwa ufadhili wa CONCERN WORLD WIDE,ambapo utakuwa unahudumia zaidi ya kaya 80 za kijiji hicho.

Friday, March 16, 2012


 ASHTAKIWA KWA KOSA LA MAUAJI
Mkazi wa kijiji cha chivu wilayani Ngara mkoani kagera amefikishwa katika mahakama ya wilaya hiyo kwa kosa la mauaji.

Mshitakiwa  Laurian Philemon  mwenye umri wa miaka 27 mkazi  wa kijiji cha  chivu  wilayani Ngara  anatuhumiwa kutenda kosa hilo  march 7 mwaka huu majira ya  saa nne usiku kijijini hapo

Mbele ya mlinzi wa amani bw Andrew kabuki, mwendesha mashitaka wa Polisi Bw Tumaini Mumbi amesema mshitakiwa anadaiwa kumuua Bi, Marysiana Leonard aliyekuwa mkazi wa kijiji cha chivu

Mshitakiwa hakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa alikuwa mbele ya mlinzi wa amani ambapo amepelekwa  rumande  na kesi hiyo itatajwa  tena  march 29 mwaka huu.


Thursday, March 15, 2012

                  
Mtangazaji wa Redio Kwizera SEIF OMAR UPUPU akizishangaa zana zilizokuwa zikitumika  zamani alipotembelea moja ya banda katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika katika viwanja vya posta wilayani Ngara.

Wednesday, March 14, 2012

WAHUKUMIWA MIAKA 30 JELA


Watu wawili wamehukumiwa kutumikia kifungo cha miaka 30 jela kila mmoja baada ya kupatikana na hatia katika kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha

Hakimu wa mahakama ya wilaya ya Ngara Bw Idrisa Katela ametoa hukumu hiyo dhidi ya Athumani Edd mkazi wa Nakatunga na Ladsilaus Onesimo mkazi wa kabanga wilayani Ngara

Awali mwendesha mashitaka wa Polisi Bw Tumaini Mumbi alisema washitakiwa walimchoma kisu kifuani Bw Lusinzi Sebabili na kumpora pikipiki yake na kuificha kwa Cosmas Reveliani mkazi wa  kabanga

Hata hivyo Mshitakiwa Cosmas Relevian ameachwa huru baada ya kukosekana kwa ushahidi dhidi yake 
"VIJANA NGARA ACHENI USHABIKI WA VYAMA VYA SIASA,TUJIPANGE            KUELEKEA MCHAKATO WA KATIBA MPYA."


Vijana wilayani Ngara mkoani Kagera,wametakiwa kuacha ushabiki wa vyama vya siasa na badala yake wajitokeze kwa wingi kutoa maoni yao kuhusu uundwaji wa katiba mpya,pindi muda utakapofika wa kufanya hivyo.

Rai hiyo imetolewa na katibu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi UVCCM wilayani Ngara Bw.Joseph Milenzo,alipokuwa akiongea na mwandishi wa habari hizi.

Amesema kwa sasa vijana wengi wameingia katika ushabiki wa kisiasa,hali ambayo inaweza kusababisha kutolewa kwa maoni ya kishabiki mpaka kupelekea katiba mpya isiwe na maslahi kwa vijana

Bw. Milenzo amesema kuwa katiba ndio muongozo wa taifa,hivyo vijana wajitokeze  kutoa maoni sahihi ili katiba itakayoundwa iweze kukidhi mahitaji yao.                                                                                   

Katibu huyo wa UVCCM ameonyeshwa kukerwa sana na tabia za baadhi ya vijana wengi kuwa mashabiki wa vyama vya siasa hasa upinzani,huku wengi wao wakiwa hawana sababu za msingi zaidi ya ushabiki tu.