Tuesday, April 17, 2012

MVUA SIKU TATU MFULULIZO

Eneo kubwa la wilaya ya Ngara kwa siku tatu mfululizo limekuwa likitawaliwa na hali ya hewa ambayo sio nzuri sana.

Asubuhi ukiamka ukungu umetanda sehemu zote na manyunyu yasiyoonyesha dalili ya kukatika.

Hii imepelekea baadhi ya watu kusimamisha shughuli zao sanasana wale wa usafiri wa boda boda na sekido.

Hiyo ndo hali halisi inayoendelea hapa Ngara ambapo kwa muda wa siku tatu jua limekuwa adim sana.

No comments:

Post a Comment