Lori hilo lenye namba za usajiri T 700 BFS lilianguka majira ya saa nane mchana siku ya jumapili April 15 katika kijiji cha Murugarama eneo la Njiapanda ya Rulenge,ambapo lilikuwa likipeleka mahindi nchini Burundi,na baada ya kuanguka lilifunga barabara hiyo hali iliyopelekea magari mengi hasa malori kukosa njia ya kupita kwa masaa kadhaa.
Watu walioshuhudia ajali hiyo wamesema kuwa chanzo chake ni mwendo wa kasi wa gari hilo,pamoja na mvua iliyokuwa ikinyesha kwa muda mrefu katika eneo hilo na kusababisha utelezi.
Hata hivyo watu waliokuwa katika gari hilo walisalimika ambao ni dereva na utingo.
Gari hilo awali likuwa likimilikiwa na Bw.Tenth Maruhe mkazi wa mjini Ngara kabla ya kuliuza kwa Mbarakk wa Biharamulo.
jitihadazikiendelea za kuliondoa barabarani |
hivi ndivyo lilivyokaa baada ya kuanguka |
wananchi wakishirikiana kuinua tela la lori hilo |
No comments:
Post a Comment