Wednesday, March 14, 2012

"VIJANA NGARA ACHENI USHABIKI WA VYAMA VYA SIASA,TUJIPANGE            KUELEKEA MCHAKATO WA KATIBA MPYA."


Vijana wilayani Ngara mkoani Kagera,wametakiwa kuacha ushabiki wa vyama vya siasa na badala yake wajitokeze kwa wingi kutoa maoni yao kuhusu uundwaji wa katiba mpya,pindi muda utakapofika wa kufanya hivyo.

Rai hiyo imetolewa na katibu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi UVCCM wilayani Ngara Bw.Joseph Milenzo,alipokuwa akiongea na mwandishi wa habari hizi.

Amesema kwa sasa vijana wengi wameingia katika ushabiki wa kisiasa,hali ambayo inaweza kusababisha kutolewa kwa maoni ya kishabiki mpaka kupelekea katiba mpya isiwe na maslahi kwa vijana

Bw. Milenzo amesema kuwa katiba ndio muongozo wa taifa,hivyo vijana wajitokeze  kutoa maoni sahihi ili katiba itakayoundwa iweze kukidhi mahitaji yao.                                                                                   

Katibu huyo wa UVCCM ameonyeshwa kukerwa sana na tabia za baadhi ya vijana wengi kuwa mashabiki wa vyama vya siasa hasa upinzani,huku wengi wao wakiwa hawana sababu za msingi zaidi ya ushabiki tu.

No comments:

Post a Comment