Friday, March 16, 2012


 ASHTAKIWA KWA KOSA LA MAUAJI
Mkazi wa kijiji cha chivu wilayani Ngara mkoani kagera amefikishwa katika mahakama ya wilaya hiyo kwa kosa la mauaji.

Mshitakiwa  Laurian Philemon  mwenye umri wa miaka 27 mkazi  wa kijiji cha  chivu  wilayani Ngara  anatuhumiwa kutenda kosa hilo  march 7 mwaka huu majira ya  saa nne usiku kijijini hapo

Mbele ya mlinzi wa amani bw Andrew kabuki, mwendesha mashitaka wa Polisi Bw Tumaini Mumbi amesema mshitakiwa anadaiwa kumuua Bi, Marysiana Leonard aliyekuwa mkazi wa kijiji cha chivu

Mshitakiwa hakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa alikuwa mbele ya mlinzi wa amani ambapo amepelekwa  rumande  na kesi hiyo itatajwa  tena  march 29 mwaka huu.


No comments:

Post a Comment