Wednesday, March 14, 2012

WAHUKUMIWA MIAKA 30 JELA


Watu wawili wamehukumiwa kutumikia kifungo cha miaka 30 jela kila mmoja baada ya kupatikana na hatia katika kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha

Hakimu wa mahakama ya wilaya ya Ngara Bw Idrisa Katela ametoa hukumu hiyo dhidi ya Athumani Edd mkazi wa Nakatunga na Ladsilaus Onesimo mkazi wa kabanga wilayani Ngara

Awali mwendesha mashitaka wa Polisi Bw Tumaini Mumbi alisema washitakiwa walimchoma kisu kifuani Bw Lusinzi Sebabili na kumpora pikipiki yake na kuificha kwa Cosmas Reveliani mkazi wa  kabanga

Hata hivyo Mshitakiwa Cosmas Relevian ameachwa huru baada ya kukosekana kwa ushahidi dhidi yake 

No comments:

Post a Comment