Kwa wale waliozoea usafiri wa mijini,hali inakuwa tofauti wanapokuja Ngara kqwani hali ya usafiri iko tofauti kabisa.
Gari ambayo kwa sehemu nyingine hupakia watu wasiozidi wanne,hapa kwetu inaweza kupakia watu zaidi ya 12,huku wengine wakikaa kwenye buti(sehemu ya kuwekea mizigo).
Nauli kutoka Ngara mpaka Kabanga ni shilingi elfu mbili kwa mtu mmoja,na kuna wakati wanapanda watu 15 kwenye hicho hicho kigari kidogo chenye uwezo wa kubeba abiria wanne.
Seat au kiti anachokalia dereva,hulazimika kukaa watu wawili kitu ambacho ni hatari sana kwani kinaweza kusababisha ajali.
hii ndiyo hali halisi |
Kuna watu wamekuwa wakileta HIACE lakini muda c mrefu hukata tamaa kutokana na abiria kutaka kupanda gari ambalo halikai muda mrefu stand likisubiri abiria